Wednesday, 30 April 2014

MAPAMBO YA SEBULENI.

Kwa mara nyingine, tunakutana tena na mambo ya sebule zetu. Hii hasa kwa wakina mama na hata wadada. Mapambo ya sebuleni hayatakiwi kuwa mengi. Mfano picha za wanafamilia, maua na mapambo mengine machache. Sebule haitakiwi kuwa imesheheni vitu vingi kupindukia mpaka ikajaa. Vitu vichache tu vinatosha. Mfano picha, maua, kutakuwa na tv na radio na mengineyo yasiyozidi kupindukia.




 Wakati wa upambaji pia zingatia rangi utakazotumia. Rangi nyeusi kila kitu mara nyingi hua haina mvuto sana. Kuna rangi mbali mbali zenye mvuto wake kulingana na aina ya mapambo na namna unavyopangilia vitu vyako. Mfano rangi kama kahawia, rangi ya machungwa na nyinginezo.



                         


https://encrypted-tbn3.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcR91LIKa3krd2sd57yU-tLwG10pjrtN-u5ki4aDvDOfq9FjdFKjpLsPf4wS


                







                                        






                                                    

No comments:

Post a Comment